Thursday, August 6, 2015

Picha hii imezua shangwe kwa wanachadema muda huu,itizame

Picha hii inaweza kuwa ndiyo picha inayoenea kwa kasi sasa katika mitandao mbalimbali picha ambayo inamuonyesha katibu mkuu wa chama cha democrasia na maendeleo chadema Dk wilbrod Slaa akiwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho ambapo imeelezwa kuwa ni baada ya kikao cha mashauriano ya kumshauri katibu huyo kurejea ofisini na kuendelea na majukumu yake.

Habari za chini ya kapeti zinasema kuwa kikao hicho kimemalizika na katibu huyo atarejea ofisini muda wowote kuendelea na jukumu kubwa la kupanga wagombea ubunge katika majimbo mbalimbali nchini.

Mtandao huu unafwatilia kwa ukaribu habari hizi tutawajuza zaidi

Wednesday, August 5, 2015

"ADC" Uchaguzi Oktoba ni baina ya CCM na CCM

Mwenyekiti wa Chama cha ADC Mhe. Said Miraj akizngumza na wajumbe wa mkutano huo Akizngumza wakati akifungua mkutano mkuu wa bodi ya wanachama wanaokutana jijini Dar es salaam kwa lengo la kupitisha majina ya wagombea urais wa chama hicho,mwenyekiti wa chama hicho  cha ADC Mhe. Said Mirajamesema kuwa kwa hali ilivyo sasa uchaguzi unaokuja mwezi wa kumi utakuwa kati ya ccm na ccm wenyewe huku upinzani ukiwa hauna nguvu kutokana na kuwapikea baadhi ya makada wa chama chama mapinduzi na kuwapa dhamana kubwa ndani ya vyama hivyo.
 Mwenyekiti wa Chama cha ADC Mhe. Said Miraj Akisalimiana na  mlezi wa chama hicho ambaye sasa ndiye mgombea wa urais 

zanzibar  kwa tiketi ya chama hicho wakisalimiana wakati wa 
 ufumnguzi wa mkutano huo
 Wakati macho na maskio ya watania yakiwa yanaangalia mnyukano wa kisiasa unaoendelea nchini baina ya chama cha mapinduzi na umoja wa katiba ya wananchi UKAWA nacho chama kipya kinachokuja kwa kasi chama cha ADC wameibuka na kusema kitendo kilichofanywa na vyama vya upinzani kuwachukua baadhi ya viongozi wa chama tawala na kuwapa madaraka ni muendelezo wa kuwasaliti watanzania na kuendelea kuipa nafasi CCM .
 Wajumbe wakiwa katika mkutano huo
Amesema kuwa kwa hali inayoendelea sasa nchini Tanzania ni wazi kuwa hakuna mtanzania aliye na nia ya dhati ya kuwasaidia watanzania ila ni ADC pekee kwa kuwa wao hawako tayari kuwapokea makada wa chama chochote waliokatwa na kuwapa madaraka kwani nao ndio wanaweza kuwarudisha watanzania tena kule ambapo wanakupinga.

Kauli hii inakuja ikiwa waziri mkuu wa zamani wa Tanzania mh EDWARD LOWASA amekihama chama chake na kuhamia cha cha democrasia na maendeleo chadema huku makada kadhaa wa chama hicho wakiendelea kukihama chama hicho na kujiunga na vyama vya upinzani.

Tizama ya magufuli leo akichukua form ya Urais

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwa sambamba na Katibu wa Itikadi na Uenezi  Taifa Nape Nnauye,Mwenyekiti wa CCM Mkoa Dar es Salaam,Ndugu Ramadhan Madabiba pamoja na pichani shoto Ndugu Januari Makamba aliyeshinda kura za maoni CCM jimbo la Bumbuli kwa pamoja wakimsindikiza Dkt Jonh Pombe Magufuli kuchukua fomu za kuwania Uraisi mapema leo jijini Dar.
   Mwenyekiti wa CCM Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwashukuru wananchi na Wanachama wa chama hicho walioshiriki shughuli nzima ya kumsindikiza Dkt John Pombe Magufuli ya kuchukua fomu ya kuwania kiti cha Uraisi kupitia chama hicho katika ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijini Dar leo.
 Mgombea Mteule wa Urais wa chama cha Mapinduzi,Dkt Jonh Pombe Magufuli akiwa kwenye gari la wazi akiwapungia mkono wananchi na wafuasi wa chama hicho nje ya Ofisi ndogo ya Makao Makuu  ya CCM mtaa wa Lumumba wakishangilia wakati Mgombea alipokuwa ikielekea ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuchukua fomu ya kuwania Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama hicho.
 Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM Dkt John Pombe Magufuli na Mgombea Mwenza Mhe Samia Suluhu Hassan nwakilakiwa na Mwenyekiti wa CCM Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wengine akipokewa katika ofisi ndogo ya CCM Mtaa wa Lumumba jijini Dar es salaam baada ya kutoka Tume ya Uchaguzi kuchukua Fomu za kugombea Urais  leo agosti 4, 2015.

Monday, August 3, 2015

Mauzauza kura za Maoni

Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi wa kura za Moniwa Kata ya Kisukulu B,Christopher Masinde akionyesha kadi ya mpigakura halali kwa wajumbe wa mkutano huo jana wakati wa kuhakiki majina kabla ya kupiga kura kuchagua wagombea udiwani na ubunge kwenye jimbo la Segerea ,Dar es Salaam .Picha|SALIM SHAO 
Mauzauza jana yalitawala mchakato wa kura za maoni kwa ajili ya kupata wagombea ubunge na udiwani kwa tiketi ya CCM kutokana na kuwapo kwa vitendo vya rushwa, vurugu, kura kuchomwa moto, makada kukamatwa, wanachama kutoruhusiwa kupiga kura na kugundulika kwa karatsi zilizokwishapigwa kura.
Kwenye baadhi ya maeneo kazi hiyo iliahirishwa hadi leo kutokana na vifaa kuchelewa na pia tatizo la kugundulika kwa shahada ambazo zimeshapigwa kura zikiwa ndani ya maboksi.
Lakini matukio yaliyotawala kura za maoni ni makada kukamatwa kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa kwa kugawa fedha au kuchapisha karatasi bandia za kupigia kura. Chanzo-Mwananchi.

RAIS KIKWETE AREJEA NYUMBANI BAADA YA ZIARA RASMI YA KISERIKALI NCHINI AUSTRALIA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Raymond Mushi katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa Jumamosi Agosti 1, 2015 mara baada ya kurejea kutoka  Australia kwa mwaliko rasmi wa Kiserikali kutoka kwa Gavana Mkuu wa nchi hiyo  Mheshimiwa Peter Cosgrove.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Saidi Meck Sadik baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa Jumamosi Agosti 1, 2015  akitokea  Australia alikozuru kwa mwaliko rasmi wa Kiserikali kutoka kwa Gavana Mkuu wa nchi hiyo  Mheshimiwa Peter Cosgrove.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda na viongozi wengine waliofika kumpokea alipowasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa Jumamosi Agosti 1, 2015  akitokea  Australia alikozuru kwa mwaliko rasmi wa Kiserikali kutoka kwa Gavana Mkuu wa nchi hiyo  Mheshimiwa Peter Cosgrove.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Dar es salaam Ndg. Ramadhani Madabida  alipowasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa Jumamosi Agosti 1, 2015  akitokea  Australia alikozuru kwa mwaliko rasmi wa Kiserikali kutoka kwa Gavana Mkuu wa nchi hiyo  Mheshimiwa Peter Cosgrove. 
PICHA NA IKULU
……………………
Akiwa nchini Australia Rais Kikwete alikutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Australia, Bwana Tony Abbot ambaye alimpongeza kwa kuamua kukabidhi madaraka kwa kiongozi mwingine kwa mujibu wa  Katiba nchini Tanzania.
Rais Kikwete pia alikutana na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake  Gavana Mkuu wa Australia Mheshimiwa Peter Cosgrove, kabla ya kukutana na wawekezaji wakubwa wa Australia ambao tayari wanawekeza nchini Tanzania ambapo walizungumzia  namna ya kuendeleza sekta mpya ya gesi nchini na jinsi Tanzania inavyoweza kunufaika  kutokana na kupata gesi.
Tayari Serikali ya Australia na makampuni binafsi ya gesi na mafuta, yanaisaidia Tanzania hasa katika vyuo vya ufundi stadi VETA na  tafiti mbalimbali katika Kilimo.
Rais Kikwete alihitimisha ziara yake kwa kutunukiwa digrii ya udaktari wa heshima ya Sheria kutoka Chuo Kikuu cha Newcastle, kwa mchango wake mkubwa alioutoa katika uongozi kwa kipindi cha miaka 10 aliyokaa madarakani nchini Tanzania na Dunia kwa ujumla.

Thursday, July 30, 2015

Umeskia Alichosema LISSU

MBUNGE wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Tundu Lissu, amesema chama chao kinatarajia kupata wanachama wengi baada Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa kujiunga na chama hicho.

Lissu ametoa kauli hiyo baada ya kuwepo taarifa kwamba wapo wanachama wa Chadema ambao watakihama chama hicho kutokana na kutokubaliana na ujio wa Lowassa ndani ya Chadema.

Akizungumza leo na waandishi wa habari Lissu amesema, “Kama wapo watakao jiondoa Chadema, wengi zaidi watakuja. Tupo katika kipindi ambacho hatujawahi kuwepo tangu mfumo wa vyama vingi uanze.

Mfumo tawala unabomoka vipande vipande. Unapo bomoka, dalili zake ni watu ambao wamekuwa katika mfumo huo kuondoka kama alivyofanya Lowassa.”
“Mabadiliko katika nchi yanatokea pale mfumo tawala unapo pasuka. Lowassa ni mfano mzuri.

Tunamkaribisha kwetu sio kwa sababu ni mwanasiasa msafi. Tumempokea kwa sababu tunaongeza nguvu kubwa kwa wale wanaotaka mabadiliko. Imetokea Zambia Mawawi, Nigeria na Kenya,” amesema Lissu.

Akizungumza kuhusu Chadema kumtuhumu Lowassa kwamba “ni fisadi” kabla ya kujiunga na chama hicho Lissu amesema, “…hatukuwa na makosa hata kido kumweka Lowassa katika kundi la watuhumiwa wa Richmond. Mambo yalizungumzwa bungeni. Aliwajibika na amesema mwenyewe aliwajibika.”

“Alijiuzuru uwaziri mkuu kwa sababu ya Richmond. Tulimweka katika orodha ya mafisadi kwa sababu ya Richmond. Na jana alisema alimwambia rais “tuvunje mkataba” rais akaataa. Angefanyeje?. hilo ni vumbi, litakapo tulia Chama Cha Mapinduzi na mfumo tawala utakuwa umeanguka, tutajenga nchini.Bila kuvunja mfumo tawala hakuna kusonga mbele,” ameeleza Lissu.

Sunday, July 26, 2015

Mwanamuziki 'Bongo Fleva' Khadija Shabani 'Keisha' ashinda CCM

MSANII wa Bongo Fleva, Khadija Shabani Taya 'Keisha' ameibuka mshindi kwenye kura za maoni za Ubunge wa viti maalum kundi la Walemavu MKoa wa Dodoma na kuwa mshindi wa kwanza.
Keisha amepata kura 340 huku Stella Fueda akiibuka na kura 112, Anna Fungo kura 100 na Graceana Kavishe kura 54.

Jumla ya kura 721 zilipigwa ambapo kura 75 ziliharibika na kura za halali zilikuwa 646.

Msanii huyo aliwahi kuhojiwa na vyombo vya habari na kubainisha kuwa japo ni mlemavu wa ngozi lakini anajikubali anajipenda kujiamini na amekuwa akipigania amani ambayo wanastahili kuipata kutoka nchini.

Alisema alipoanza kuweka picha zake za siasa kwenye mtandao kuna baadhi ya watu walimpongeza na wapo waliosema kuwa hana uchungu na wenzake kwani waliamini anaingia kwenye siasa kwa nia ya kujinufaisha “Wapo wanaohisi nimeingia huku kwa ajili ya kujinufaisha mwenyewe mimi
ni mpiganaji na ndomana siku zote nimekuwa nikiwaza kuhusu amani yetu” alisema.

Alisema fimbo ya mbali haiui nyoka na kidole kimoja hakivunji chawa akimaanisha kuwa lazuima kusimamia sheria ambazo zitatusaidia kuendeleza amani hivyo basi lazima kuwe na wawakilishi wa kutosha ndani ya bunge ili sauti zisikike ili sheria kutungwa na kutekelezwa pia.
  • Taarifa ya Sifa Lubasi, Dodom 
  • Habari za asubuhi ndugu zangu rafiki zangu mashabiki zangu na media zote nchini.najua wengi mnajiuliza maswali mengi sana juu yangu kwanini nimeamua kuingia kwenye siasa lakini leo naomba nifunguke na kuwaambia kitu.

    Mimi kama mlemavu wa ngozi najikubali najipenda na ninajiamini lakini yote tisa napigana kwa uhuru na amani ambayo tunastahili kuipata kutoka nchini kwetu.

    Nilipoanza kupost picha zangu za siasa kuna ambao walinipongeza na kuna ambao walinisema kwamba sina uchungu na wenzangu kwakuwa wanahisi nimeingia huku kwa ajili ya kujinufaisha mwenyewe mimi ni mpiganaji na ndomana siku zote nimekuwa nikiwaza kuhusu amani yetu.fimbo ya mbali haiui nyoka na kidole kimoja hakivunji chawa nikimaanisha kwamba lazima tusimamie sheria ambazo zitatusaidia kuendeleza amani hivyo basi lazima tuwe na wawakilishi wa kutosha ndani ya bunge ili sauti zetu zisikike ili sheria kutungwa na kutekelezwa pia.hivyo mimi kama mtanzania mwenzenu nahitaji support yenu ili niweze kufikia malengo yetu kwa yeyote ambaye anaupendo nasi na mimi na harakati zangu anisaidie kwa chochote ambacho kitanifikisha nnapoataka.

    this is my tigo no 0718785045 na hii ni account number yangu ya crdb 011 2022295800 jina ni hadija shabani Taya unaweza kuchangia humo na kwa upendo kabisa naomba u repost hii post kadri muwezavyo ahsanteni shukrani.