Thursday, May 24, 2018

DAWA ZAVUSHWA KUPITIA MTO WENYE MAMBA MKOANI RUVUMA

WANANCHI wanaoishi katika Vijiji vya Mkenda na Mitomoni vilivyopo kandokando ya mto Ruvuma wilayani Nyasa mkoani Ruvuma wamesema changamoto kubwa waliyonayo ni 
mazingira magumu ya miundo mbinu ambayo inasababisha ugumu wa ufikishaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara kutoka  Bohari ya Dawa (MSD).

Wakazi hao wamesema kuwa, mazingira ya kufikisha dawa kwenye vijiji hivyo hutegemea zaidi usafiri wa kuvuka mto Ruvuma ambapo hulazimika kutumia boti,ambapo hata hivyo maisha yao yanakuwa na mashaka ndani ya mtumbwi hiyo ambayo iko wazi kutokana na mto huo kuwa na mamba wengi.

"Changamoto yetu kubwa ni usafishaji wa dawa kuja hapa kijijini kutokana na kutegemea zaidi mto huu ambao una mamba wengi, hata mwaka huu mwanzoni mtumbwi huu mnaouona ulipinduka na watu  wakiwapo wauza mitumba waliuawa na mamba; lakini tunashukuru  Bohari ya Dawa (MSD) kwani wao wanaweza kutuletea dawa  kwa wakati" alisema Mwenyekiti wa kamati ya Afya wa kijiji cha Mitomoni Omar Hassan.

Alisema ili kuondoa changamoto hiyo, wanaiomba serikali kuhakikisha inaboresha miundombinu ya barabara, ili dawa hizo zisafirishwe kwa njia ya barabara badala ya kutegemea mto huo. 

Alisema yeye na kamati yake wamekuwa wakipokea dawa mara nne kwa mwaka kutoka MSD na kuzihakiki kwa ajili ya matumizi.

"Pamoja na changamoto ya miundombinu lakini tumekuwa tukihakikisha dawa zinazoletwa na MSD zinafika kituoni na kutumika ipasavyo,"alisema.

Alisema kutoka Songea mjini hadi Kijiji cha Mitomoni, Songea vijijini, katika kituo hicho cha afya ni km 135 na MSD imekuwa ikihakikisha dawa hizo zinafika.

Alisema changamoto zinakuwa kubwa zaidi kipindi cha mvua kwa kuwa miundombinu ya barabara hadi kufika kivukoni ni tatizo na kuna wakati dawa zinafika usiku na zinatakiwa kuvushwa usiku huo huo.

Hassan alisema changamoto hiyo ya mamba katika mto huo anaijua vizuri kwani mtoto wake Sanifu Omar (27), alipoteza maisha kwa kuliwa na mamba wakati alipokuwa akisafirisha abiria kwa kutumia mtumbwi.

Mkazi wa Kijiji cha Mitomoni Khadija Salum alisema wamekuwa wakipata dawa zote muhimu katika kituoni hicho ikiwemo za mama mjamzito na mtoto bila ya ubaguzi na kwa wakati.

"Mimi nina watoto watano kuanzia ujauzito wa kwanza sijawahi kukosa dawa hapa pamoja na ugumu wa miundombinu lakini dawa zinafika hivyo serikali ione haja ya kuboresha barabara zetu," alisema.

Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Mitomoni, Ivo Hekela, alisema kijiji hicho kinahudumia agonjwa 12,000 kutoka vijiji vitano ambavyo ni Mitomoni, Mipotopoto,Konganywita,Mkenda,Uhuru na Mozambique. 

Meneja wa MSD Kanda ya Iringa, John Sipendi, alisema wamekuwa katika changamoto ya kufikia vituo hivyo vya pembezoni ikiwa ni pamoja na kutumia muda mrefu kufikisha dawa na wakati wa mvua kukwama kwa magari njiani na gharama za usafirishaji kuogezeka.

Madereva wa MSD Kanda ya Iringa wamesema wamekuwa wakishindwa kushusha dawa wakati wa mvua za masika kutokana na mto huo kujaa maji hivyo hulazimika kulala kijijini hapo kwa siku mbili hadi tatu.

Tanzania yaombwa kuisaidia Palestina

Kamati ya Mshikamano wa Tanzania na Palestina imeitaka Tanzania kuendelea kushawishi Umoja wa Mataifa kuleta mapatano kati ya Paletina na Israel ili Wapalestina waweze kuwa na Amani katika nchi yao kama ilivyo kwa Watanzania.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Ndugu Abdullah Othman wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Juzi jijini Dar es salaam na kusema kuwa tunapozindua ubalozi huko Tel Aviv nivizuri tukakumbuka majanga yanayowapata wenzetu Wapalestina wanaoendelea kukandamizwa na Tukumbuke msimamo aliokuwanao Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere ambae mnamo 1984.

Othmani alisema kuwa kwa Tanzania kufungua Ubalozi wake huko Israel mjini Tel Aviv na kuikaribisha Israel nayo ifungue ubalozi wake nchini Tanzania hakuna pingamizi na hilo bali tunahofia Misimamo iliyosifika nayo Tanzania Kimataifa kudhoofika.

Tunaambiwa yote haya yanatokana na sera yetu mpya ya Diplomasia ya Kiuchumi inayolenga mahusiano yenye maslahi yakiuchumi na nchi yoyo teduniani. Hatuna pingamizi nahilo ila tunatahadharisha isitupeleke kuja kuregeza misimamo yetu madhubuti iliotupaheshima katika anga za kimataifa na misimamo ilioasisiwa na Baba wa Taifa,nayo nikupinga Ukandamizwaji,Uonevu na Ukoloni mambo leo” alisema Othman.
[​IMG]
Pia Othmani aliitaka Serikali kutafakari kwa kina aina gani ya Mahusiano inayojenga kati ya Tanzania na Palestina kwa hatua yake ya kufungua Ubalozi Israel Mjini Tel Aviv na kuikaribisha Israel nchini nayo ifungue Ubalozi wake kwa mlango wa sera mpaya ya Kiuchumi.

Je leo hii katika kipindi hiki tunafungua ubalozi kwa sera mpya ya Kiuchumi na  watajisikiaje ? haliyakuwa  Israel ambayo imewatia gerezani Wapalestina zaidi ya 6,000, wakiwemo watoto 304 na wanawake 63. Hawa ni wafungwa wa kisiasa ambao wamefungwa chini ya sharia yakijeshi. Idadi yao inazidi kuongezeka kila siku.
 Image may contain: 3 people, people smiling
Siku moja baada ya Tanzania  kuzindua Ubalozi wake Israel, Wapalestina  zaidi ya 50 wameuwawa wakiandamana wakiwemo watoto na wanahabari wawili dhidi ya hatua ya Marekani kufungua ubalozi Jerusalem, Zaidi ya Wapaletina 5,500 wamejeruhiwa. Sikumoja tu!

Monday, May 21, 2018

Jumuiya ya Waislamu Shia Ithnasheriya Tanzania yaftari na Kamati ya Amani ya Mkoa wa Dar es salaam.

Kiongozi Mkuu wa Waislam Shia Ithnasheriya Tanzania Maulana Sheikh Hemed Jalala akiongea katika hafla ya futari ya pamoja na Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es salaam, Masjid Ghadir Kigogo Post Dar es salaam.
Kiongozi Mkuu wa Waislam Shia Ithnasheriya Tanzania Maulana Sheikh Hemed Jalala Amewataka Watanzania, Waislamu na Wakritso kuwa na Umoja wa dini zote kwa kurudi katika mafundisho ya Dini zao Quran na Injiri.

Sheikh Jalala amesema hayo jana katika hafla ya Futari ya Maoja na Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es salaama, iliyoandaliwa na Jumuiya ya Waislamu Shia Ithnasheriya Tanzania Makao Makuu ya Jumuiya hiyo, Masjid Ghadir, Kigogo Post Dar es salaam na kuwasisitiza Watanzania, Waislamu na Wakristo kudumisha amani, maelewano na masikilizano kwa kuzilia Nafsi zao kwa kumtambua Mwenyezi Mungu vizuri pamoja na Vitabu vyao.

“Katika tunu tunaoililia leo katika nchi yetu ya Tanzania nchi ya watu ambao ni wamaoja, wamekuwa wanaishi pamoja bila kubaguana hata siku moja, wala hawajuani kwa makabila yao, Umoja wa Dini zote ziliopo nchini Tanzania na dini kubwa tulizonazo ni Uislamu na Ukristo, naamini ya kwamba Waislamu na Wakristo wanaweza kuwa kitu kimoja watakaporudi kwenye Vitabu vyao Quran na Injiri vinasemaje” Alisema Sheikh Jalala

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Waislamu Shia Ithnasheriya Tanzania Sheikh Issa Rwechungura akiongea katika hafla ya futari ya pamoja na Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es salaam, Masjid Ghadir Kigogo Post Dar es salaam.
Nae Mwenyekiti wa Jumuiya ya Waislamu Shia Ithnasheriya Tanzania Sheikh Issa Rwechungura amesema baadhi ya Wafuasi wa dini ya Kiislamu wamekuwa hawafuati muongozo wa dini ya Kiislamu na hatimae kuwa chanzo cha mifarkano katika Jamii inayowazunguka.

“Tunalazimika kufuata Muongozo wa Dini ya Kiislamu baada ya kuwa tumesilimu, tatizo ndugu zangu ni kwamba baadhi yetu katika waislamu hatuambatani na muongozo wa Dini ya Kiislamu na matokeo yake inatokea Mifarakano kati yetu au kati yetu na wasiokuwa Waislamu, kinyume kabisa na mafunzo ya Mtume Muhammad (s.a.w.w)” alisema Sheikh Rwechungura.

Sheikh Rwechungura amesema kuwa swala la makundi katika jamii yetu ni jambo ambalo lipo na haliepukiki, bali wajibu wetu ndani ya jamii  hususani ya Kitanzania ni kutafuta muafaka wa kuishi kwa amani ili amani hiyo ituwezeshe kutekeleza majukumu yetu ya kirofo na ya Kijamii.

Mwenyekiti wa Taasisi ya Al Bukhar Foundation Sheikh Khalifa Khamisi akiongea katika hafla ya futari ya pamoja na Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es salaam, Masjid Ghadir Kigogo Post Dar es salaam.
Hatahivyo Kwaupande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Al Bukhar Foundation Sheikh Khalifa Khamisi amewataka Watanzania kipindi hiki cha Mfungo wa Ramadhani kupeleka mawazo na akili kwa wenzetu Wapalestina kwani kwani hawapo katika amani na utulivu.

“Ili tuishi kwa usalama tunaweza kujifunza zaidi katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani Watanzania na Waislamu kwa ujumla sote tupeleke akili zetu na mawazo yetu kwa wenzetu wapalestina, Taifa la Palestina ni taifa ambalo limetekwa, limechukuliwa na Mazayuni (Mayahudi) imewadunisha na kuwadhalilisha Waislamu, Wakristo na Wapalestina wanaoishi katika taifa hilo, wakati sisi tuko hapa katika hali ya amani tukilindwa na askari ambao hawana silaha, wenzetu Wapalestina, Waislamu na Wakristo waishio Palestina wanazungukwa na askari wenye silaha na anaepinga amri anauwawa” Amesema Sheikh Khamisi

Sheikh Khamisi amesema kuwa moja ya leongo la Funga ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni ili mwanadamu aweze kusalimika na Vishawishi vya Mwili, uweze kuwa na udhibiti tama za mwili na ili muweze kujifunza namna bora zaidi ili Watu waishi kwa Amani.

Sunday, May 20, 2018

"Tunazindua Ubalozi Tel Aviv wakati Wapalestina wanaomboleza miaka 70 ya Kuvamiwa:?" Abdallah Othman


Image may contain: 3 people, people smiling
Uzinduzi/ Ufunguzi rasmi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Israel leo tarehe 08/05/2018. Shughuli hiyo imefanywa na Mhe Waziri wa Mambo ya Nje Balozi Augustine Mahiga pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Israel Mhe Job Masima. Ubalozi huo wa Tanzania ulitambuliwa rasmi mwezi Mei 2017.

KAMATI YA MSHIKAMANO WA TANZANIA NA PALESTINA

Tamko kwa Umma
Tunazindua ubalozi Tel Aviv wakati Wapalestina wanaomboleza miaka 70 ya Nakba
(Janga au Kuvamiwa)

HATIMAYE nchiye tuimefungua ubalozi wake huko Israel. Waziri wa mambo yanje na uhusiano wakimataifa Dk. Augustine Mahiga amezindua ubalozi huo mjini Tel Aviv na kuikaribisha Israel nayo ifungue ubalozi wake nchini Tanzania.  

Tunaambiwa yote haya yanatokana na sera yetu mpya ya Diplomasia ya Kiuchumi inayolenga mahusiano yenyemaslahi yakiuchumi na nchi yoyo teduniani. Hatuna pingamizi nahilo ila tunatahadharisha isitupeleke kuja kuregeza misimamo yetu madhubuti iliotupaheshima katika anga za kimataifa na misimamo ilioasisiwa na Baba wa Taifa,nayo nikupinga Ukandamizwaji,Uonevu na Ukoloni mambo leo.

Ndipo tunajiuliza, hivi enzi zile za utawala wa makaburu kule Afrika Kusini tuliwasusia na kuwalaani kwasababu hatukuhitaji misaada au kwasababu ya msimamo wetu dhidi ya ukoloni na ukandamizaji?

Ufunguzi wa ubalozi tunasikitika umekuja katikakipindi kibaya, mwezi ambao ndugu zetu Wapalestina wanaadhimisha miaka 70 ya NAKABA, au JANGA, wakati ambapo nchi yao ilivamiwa na Wayahudi na wao kufukuzwa na kufanywa wakimbizi.

Wapalestina mwezi huu wote wanaandamana kupinga uporaji wa ardhi yao na uonevu wanaofanyiwa na kuuliwa bila hatia yoyote.Hiki kilikuwa siokipindi MUWAFAKA cha kufungua Ubalozi wetu kwambwembe zilezilokuwako. Huko nikuwatia unyonge nahuzuni ndugu zetu hao Wapalestina.
Kiongozi wa Wapalestina Yasser Arafat

Safari ya kwanza ya Kiongozi wa Wapalestina Yasser Arafat hapa Tanzania na alipokutana na Kamati ya Mshikamano ya Tanzania na Palestina aliwambia maneno haya, na nanukuu:

“Tulipokuwa katika mapambano yakuzuwia mauwaji yasio na hatia yanayofanywa na Askari wa ISRAEL kwa wakimbizi wa Kipalestina waliopo katika makambi ya SABRA na SHATILA tulipata faraja kubwa kusikia ndugu zetu wa Tanzania wanaandama na kulaani kwanguvu zote mauwaji hayo wakati Ulimwengu umekaa kimya na hata ndugu zetu wa nchi za Kiaarabu wako kimya. (Tanzania) ilikuwa ninchi ya kwanza ulimwengu kufanya hivyo kwakweli tulifarijika.”

Je leo hii katika kipindi hiki tunafungua ubalozi kwambwembe watajisikiaje ?
Hii ni Israel ambayo imewatia gerezani Wapalestina zaidi ya 6,000, wakiwemo watoto 304 na wanawake 63. Hawa ni wafungwa wa kisiasa ambao wamefungwa chini ya sharia yakijeshi. Idadi yao inazidi kuongezeka kila siku.

Je sisi Watanzania tuna msimamo gani? Au nisuala la “maslahi ya kiuchumi” tu?
Wapalestina zaidi ya 51 waliuwawa na Askari wa Israel katika nchi yao mnamo 14 Mei 2018, Gaza

Watanzania tunaungana na Wapalestina katika siku hii ya maadhimisho ya NAKABA,kwa sababu mwaka 1948 majeshi ya Kizayuni yaliteketeza vijiji na miji ya Wapalestina zaidi ya 530,na kuwafukuza Wapalestina 750,000 kutoka nchi yao ya  Palestina kwa mtutu wa bunduki 

Wapalestina takriban 750,000 wakaporwa asilimia 78 ya ardhi yao na kugeuzwa wakimbizi. Wapalestina zaidi ya 15,000 waliuliwa.
Hili ni janga kubwa katika historia na maisha ya Wapalestina. Kwa Kiarabu wanatumia neno “Nakba”. 
[​IMG]
Kwa mujibu wa takwimu za utawala wa Kizayuni wa Israel kuna watoto 437 Wapalestina wanaoshikiliwa kwenye jela za utawala huo.

Hivi ndivyo nchi ya Palestina ilivyofutwa katikar amani ya dunia na badala yake wakabuni nchi yaIsrael kwa ajili ya Wayahudi. Na hivi ndivyo wanavyosheherekea “uhuru” waokila mwaka. Je, tuna msimamo gani kuhusu Nakba?

Leo hii zaidi ya Wapalestina milioni saba wamelazimishwa kuwa wakimbizi wakiishi katika nchi mbalimbali duniani. Wengi wao wanaishi katika kambi za wakimbizi katika maeneo ya Ukingo wa Magharibi, Ukanda wa Gaza, Lebanon, Jordan, Syria na kadhalika.
Wakimbizi hawa wanazuiwa na Israel kurudi makwao kwamjibu wa sharia ya kimataifa na maazimio ya Umoja wa Mataifa. Katika Gaza maelfu wamekuwa wakiandamana kwa muda wa miezi miwili sasa wakidai haki yao ya kurudi walikofukuzwa tangu 1948.

 Matokeo yake nikupigwa risasi za moto na wanajeshi wa Israel.
 Siku moja baada ya Tanzania  kuzindua ubalozi, Wapalestina  zaidi ya 50 wameuwawa wakiandamana dhidi ya hatua ya Marekani kufungua ubalozi Jerusalem. (wakiwemo watoto na wanahabari wawili). Zaidi ya 5,500 wamejeruhiwa. Sikumoja tu!
Hivyo, Nakba iliyo anza miaka 70 iloyopita (mwaka 1948) ingali inaendelea hadi leo. Kila siku Wapalestina wamekuwa wakikabiliana na risasi za moto, vifaru, ndege za kivita na makombora. 

Makazi yao na mashamba yao yamekuw ayakiteketezwa,  ardhi zao zinaporwa, wanakamatwa na kufungwa katika magereza chini ya sharia za kijeshi. Hivyo haku na Mahakama wala mashtaka bali huteswa na kudhalilishwa. Ni pamoja na watoto na wanawake   
Wazayuni wanadai bila aibu kuwa wanafanya yote haya eti “kujilinda”.

Leo hii tunapozindua ubalozi huko Tel Aviv nivizuri tukakumbuka majanga yanayowapata wenzetu Wapalestina wanaoendelea kukandamizwa. Tukumbuke msimamo aliokuwanao Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere ambae mnamo 1984 (kabla ya kung’atuka) alisema:
Baba wa Taifa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwalimu Julias Kambarage Nyerere

“Siku zote tumekuwa na msimamo usioyumba wa kuunga mkono haki ya Wapalastina ya kujitawala. Sisi Watanzania tulipokuwa tunadai uhuru wetu tulifanya hivyo tukiwa nchini mwetu. Wapalestina hali yao ni mbaya zaidi. Ni kwasababu wameporwa nchi yao na wamekuwa taifa lisilo na nchi. Ndio maana wanastahili kuungwa mkono siyo tu na Tanzania bali na Ulimwengu mzima. Dunia lazima iwasikilize kilio chao, iwaelewe na iwaunge mkono” 

Huu ndio msimamo wa Kamati yetu. Tunatumai ungali ni msimamo wa Nchi yetu ya Tanzania.
Kuheshimu utu wa mwanadamu duniani kote imekuwa daima ni tunu ya taifa letu tangu enzi za Mwalimu. Tuendelee kutunza tunu hii ili tusije tukasaliti msimamo wa taifa hili.

Abdullah M.Othman
Mwenyekiti
Kamati ya Mshikamano wa Tanzania na Palastina
Dar es Salam                                                                                    15 Mei 2018