Monday, August 24, 2015
Sunday, August 23, 2015
ACT-Wazalendo wavuna Wanachama 500 kutoka CHADEMA
Zaidi ya wanachama 500 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
wakiwemo viongozi wa kata mbalimbali katika wilaya ya Ludewa mkoani
Njombe, wamekihama chama hicho na kujiunga na chama cha ACT-Wazalendo.
Zaidi
ya wanachama 500 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
wakiwemo viongozi wa kata mbalimbali katika wilaya ya Ludewa mkoani
Njombe, wamekihama chama hicho na kujiunga na chama cha ACT-Wazalendo.
Wanachama hao wamefikia maamuzi ya kukihama chama hicho huku wakiwalalamikia viongozi wao wa CHADEMA wilaya na taifa kumkata mgombea wao wa ubunge jimbo la Ludewa waliyemuhitaji Bwana Okol Haule na kumuweka mgombea wanayemuhitaji wao bwana Bathoromeo Mkinga.
Mamia ya wanachama hawa kutoka wilaya ya Ludewa, wamefanya maandamano ya amani kutoka mtaa wa Kilimahewa hadi katika ofisi za chama hicho zilizopo mjini Ludewa wakiwa na mabango ya aina mbalimbali yakilaani viongozi wa CHADEMA wilaya na taifa kumkata Okol Haule aliyeshinda katika kura za maoni kugombea nafasi ya ubunge katika jimbo hilo.
Hata mara baada ya wanachama hawa kuwasili katika ofisi za CHADEMA wilaya, viongozi waliingia mitini na kufunga ofisi, lakini dhamira ya wafuasi hawa wa CHADEMA wakiwemo viongozi wa juu kutoka kata mbalimbali za wilaya ya Ludewa, haikuishia hapo na wote wakiwa hawana imani tena na CHADEMA wakaelekea ofisi za ACT Wazalendo mtaa wa Sokoni na kujiunga nacho.
Huku wakidhamiria kuisambaratisha kabisa CHADEMA wilayani humo, wanachama hao wakiungana na mgombea wao wanayemuhitaji bwana Okol Haule wakachoma moto nguo aina ya kombati alizokua akizitumia mgombea huyo, bendera na kadi za CHADEMA ambapo bwana Haule anasema ameshindwa kuvumilia ubakaji wa demokrasia uliofanywa na viongozi wa CHADEMA. chanzo EATV
Wanachama hao wamefikia maamuzi ya kukihama chama hicho huku wakiwalalamikia viongozi wao wa CHADEMA wilaya na taifa kumkata mgombea wao wa ubunge jimbo la Ludewa waliyemuhitaji Bwana Okol Haule na kumuweka mgombea wanayemuhitaji wao bwana Bathoromeo Mkinga.
Mamia ya wanachama hawa kutoka wilaya ya Ludewa, wamefanya maandamano ya amani kutoka mtaa wa Kilimahewa hadi katika ofisi za chama hicho zilizopo mjini Ludewa wakiwa na mabango ya aina mbalimbali yakilaani viongozi wa CHADEMA wilaya na taifa kumkata Okol Haule aliyeshinda katika kura za maoni kugombea nafasi ya ubunge katika jimbo hilo.
Hata mara baada ya wanachama hawa kuwasili katika ofisi za CHADEMA wilaya, viongozi waliingia mitini na kufunga ofisi, lakini dhamira ya wafuasi hawa wa CHADEMA wakiwemo viongozi wa juu kutoka kata mbalimbali za wilaya ya Ludewa, haikuishia hapo na wote wakiwa hawana imani tena na CHADEMA wakaelekea ofisi za ACT Wazalendo mtaa wa Sokoni na kujiunga nacho.
Huku wakidhamiria kuisambaratisha kabisa CHADEMA wilayani humo, wanachama hao wakiungana na mgombea wao wanayemuhitaji bwana Okol Haule wakachoma moto nguo aina ya kombati alizokua akizitumia mgombea huyo, bendera na kadi za CHADEMA ambapo bwana Haule anasema ameshindwa kuvumilia ubakaji wa demokrasia uliofanywa na viongozi wa CHADEMA. chanzo EATV
Friday, August 21, 2015
Mh.Mbatia awaonya Viongozi wa UKAWA
Wakati Umoja wa Katiba
ya wananchi UKAWA ukikumbwa na changamoto ya ugawanaji wa majimbo baada ya
maeneo mengi nchini Tanzania kuibuka migogoro mara baada ya majimbo ya uchaguzi
kugawanywa kwa vyama hivyo,hatimaye mwenyekiti wa chama cha NCCR MAGEUZI ambaye
ni mwenyekiti mwenza wa umoja huo ameibuka na kutoa onyo kali kwa viongozi
ambao wanakuwa wabinafsi wa kutokutaka kuachiana majimbo na kusema kuwa
ubinafsi ni jambo ambalo halitaendekezwa ndani ya umoja huo.
Akizungumza na
wanahabari leo jioni hii Dar es salaam amesema kuwa mara baada ya kukamilika
kwa kazi ya kugawana majimbo kwa vyama vinne vinavyounda umoja huo kumeibuka
sintofahamu ya baadhi ya watu kungangania majimbo ambayo tayari wamepewa watu
wengine jambo ambalo amesema kuwa sio makubaliano ya umoja huo na hawatavumilia
viongozi wa namna hiyo.
Amesema kuwa moja ya
maazimio makubwa ya umoja huo ni kuepuka ubinafsi na kuhakikishya kuwa mambo
wanayoyahubiri kwa wananchi wanayatekeleza kwa vitendo ikiwa ni pamoja na amani
na umoja hivyo hawako tayari kuona chama au mtu yoyote anaanzisha vurugu ndani
ya umoja huo.
Amesema Tayari leo
jioni viongozi wakuu watakutana kuona ni jinsi gani wanaweza kushughulikia
jambo hilo ili ndoto za watanzania za kuhakikisha kuwa wanauondoa mfumo dhalimu
wa CCM uliopo kwa sasa zinatimia na nchi inakuwa na amani na utulivu mkubwa.
Wednesday, August 19, 2015
Mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu
Watu watatu wamekufa na wengine
thelathini wamelazwa hospitalini kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa
kipindupindu nchini Tanzania na hasa katika mji wa kibiashara wa Dar es
salaam.
Wataalamu wa afya wamesema kwamba mlipuko huo unapatikana
kwenye maeneo ambayo hayana usafi wa kutosha na vyoo vya kisasa hasa
katika maeneo yenye msongamano wa makazi katika jiji hilo.
Maafisa wa afya tayari wameshachukua hatua ili kuzuia mlipuko huo
usienee zaidi tangu mlipuko mkubwa wa kwanza ulioripotiwa kulikumba jiji
hilo mwaka 2009.
Wodi tengefu kwa wagonjwa wa ugonjwa huo
imeshaandaliwa katika hospitali za wilaya ya Kinondoni eneo ambalo
limeathiriwa vibaya na ugonjwa huo.
Umma wa watanzania wametakiwa kuwa waangalifu baada ya kifo cha
mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka ishirini na saba,mwishoni mwa wiki
iliyopita baada ya kuonesha dalili zinazoshabihiana na magonjwa ya
milipuko.
Dar es salaam ni mmoja kati ya miji yenye idadi kubwa ya watu, mji huo pekee una idadi ya watu zaidi ya milioni tano.
UTAFITI WA AFYA YA UZAZI NA MTOTO NA MALARIA KUANZA RASMI TAREHE 21 AGOSTI, 2015
Wito huo uletolewa leo na
Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt.
Ahmed Makuwani wakati wa hafla fupi ya kufunga mafunzo ya utafiti huo
iliyofanyika wilayani Moshi, Kilimanjaro.
“Ninawaomba Wananchi kutoa
ushirikiano wa kutosha kwa Wadadisi, Wasimamizi na
Wahaririwatakaoshiriki zoezi la kukusanya Takwimu za Utafiti wa Afya ya
Uzazi na Mtoto na Malaria wa mwaka 2015 ili kupata taarifa muhimu na
sahihi kwa ajili ya kupanga Mipango na Sera endelevu za Sekta ya Afya
katika nchi yetu, amesema Makuwani”.
Dkt. Makuwani amesema kuwa
taarifa zitakazokusanywa kwa wananchi kwa ajili ya utafiti huo zitakuwa
ni siri na zitatumika kwa shughuli za Kitakwimu tu na wala hazina
uhusiano wowote na Uchaguzi mkuu wa Mwaka huu.
kwa upande
wa Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa
amesema utafiti huu wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Malaria wa mwaka 2015
unalenga kukusanya taarifa nyingi za sekta ya afya zinazotumika katika
kutathmini malengo mbalimbali na pia kusaidia katika kupanga mikakati
mipya.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa
mara nyingine tena inafanya Utafiti wa Afya ya Uzazi na Mtoto na Malaria
wa mwaka 2015 ambao kwa mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2010. Utafiti
huu utaanza rasmi tarehe 21 Agosti, 2015 kwa nchi nzima na utamalizika
mwishoni mwa Mwezi Februari 2016.source.Fullshagwe
Sunday, August 16, 2015
Nasrullah aikosoa Marekani kwa kuitumia Daesh
Katibu Mkuu wa chama cha Hizbullah cha Lebanon amesema kuwa Marekani
inalitumia kundi la kigaidi la Daesh kuligawa eneo la Mashariki ya Kati.
Sayyid Hassan Nasrullah amesema kuwa Washington na waitifaki wake
wanatumia ugaidi hususan kundi la kigaidi la Daesh kama wenzo wa
kutekeleza mpango wa kuligawa eneo la Mashariki ya Kati, kuanzia Iraq
hadi Syria na hata Saudi Arabia kwa sababu mpango huo unafanyika kwa
maslahi ya Marekani na utawala wa Kizayuni.
Sayyid Hassan Nasrullah
ameyasema hayo jana usiku katika hafla ya kuadhimisha mwaka wa tisa wa
ushindi wa Muqawama wa Lebanon dhidi ya utawala wa Kizayuni katika vita
vya mwezi Julai mwaka 2006.
Katibu Mkuu wa Hizbullah amesema kuwa upo
udharura wa kupinga na kukabiliana na mpango wa kuligawa eneo hili.
Mawahabi wataka misikiti saba ya Madina ibomolewe
Mjumbe wa baraza la maulamaa wa Saudi Arabia na mmoja wa mawahabi mwenye
misimamo ya kufurutu ada ametaka misikiti saba maarufu ya Madina
ibomolewe.
Saleh al-Fawzan, mjumbe wa baraza la maulamaa wakuu wa Saudia
na mjumbe wa kamati ya kudumu ya utoaji fatuwa amedai leo kuwa misikiti
saba ya kihistoria ya mjini Madina ni bid’a na yote inapasa ibomolewe.
Historia ya misikiti hiyo saba inarejea kwenye zama za vita vya Khandaq
na iko kwenye bonde la mlima Sala’a magharibi mwa Msikiti mtukufu wa
Bwana Mtume Muhammad SAW mjini Madina.
Misikiti hiyo saba hivi sasa
imekuwa moja ya maeneo ya ziara kwa Waislamu kutoka nchi mbalimbali
duniani; ambapo mara baada ya kuwasili Madina Waislamu hao huenda kuzuru
misikiti hiyo.chanzo Irib.
Subscribe to:
Posts (Atom)








